Baada ya kupata nafasi ya kutimba Nairobi Kenya ndani ya Coke Studio,
Joe na G naoko waliitumia fursa hiyo kufanya collable na mkali kutoka
Kenya "Rabit" .Sikiliza wimbo huo "Najipendelea" hapa chini.
Mdau wa Mziki pokea kazi mpya toka kwa wakongwe hawa wawili katika kuihamasisha jamii ya ki TANZANIA kuhusu hali ya sasa na Uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015. Wimbo umefanywa Mwanalizombe Records chini ya Producer Villy.
Mwana FA aka Binamu anatarajia kuachia single mpya ‘Kiboko Yangu’, ambayo amemshirikisha Alikiba Ikiwa ni miezi mitano imepita toka aachie ‘Mfalme’. Binamu ambaye pia anatarajia kupanda kwenye jukwaa la ‘Serengeti Fiesta’ leo (October 18) akiwa na ‘surprises’ kibao, ameiambia Bongo5 kuwa Jumatano ijayo (October 22) single ya ‘Kiboko Yangu’ itakuwa tayari kwenye vituo vya radio. Kabla hajaachia ‘Mfalme’ May, 2014, Hamis Mwinjuma alikuwa amepanga aanze kutoa ‘Kiboko Yangu’ ambayo ilikuwa tayari imerekodiwa kwenye studio ya MJ Records kabla ya ‘Mfalme’, lakini mipango ilibadilika.
Ninaposikiliza track
kama hii inanirudisha kwenye harakati za ukweli za muziki ambao hivi
sasa Tanzania imeweza kuwa na mtindo wa “MUZIKI WA KIAZI KIPYA”
unaotikisa nchi nzima na kuweza kuwafikisha vijana kwenye INTERNATIONAL
AWARDS… muziki ambao “ulipingwa” kila kona katika jamii ya Mtanzania
wakati imeanza, lakini bado iliweza kushinikiza kishida shida bila
kuingiza kiasi chochote cha pesa na bila kupigwa kwenye radio yoyote
nchini, Bongo Hip Hop ilipigwa mtaani na kwenye Concerts peke yake…
Hivi sasa “HARAKATI BONGO HIP HOP” imeweza kuzaa “BONGO FLAVA” na
wasanii kuweza kuingiza kipato na imeweza kuwa ni ajira kwa vijana
nchini. (R.I.P) NIGGER ONE – ADILI KUMBUKA, D-ROB na wengine waliotutangulia
mbele ya Haki walishiriki kwenye mchakato mzima wa “Bongo HIP HOP
Movement” “Hip Hop Forever” SIKILIZA